Thursday, January 15, 2026
28.8 C
Dar es Salaam

Watu 11 wafariki, 14 wajeruhiwa katika tukio la mauaji Pretoria, Afrika Kusini

Takribani watu 11 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa baada ya tukio la ufyatuaji risasi lililotokea mapema Jumamosi asubuhi Afrika Kusini. Tukio hilo limesababisha mauaji jijini Pretoria. Kwa mujibu wa polisi, tukio hilo lilitokea majira ya saa 4:00 asubuhi katika hosteli ya Saulsville, iliyopo Atteridgeville, magharibi mwa Pretoria. Miongoni mwa waliopoteza maisha ni watoto watatu. Polisi wamedhibitisha kuwa mvulana wa miaka...

Baadhi ya Nchi Kushindwa Kupeleka Mashabiki Kombe la Dunia 2026

Huu ni muhtasari wa nchi zinazoweza kushindwa kupeleka mashabiki nchini Marekani kutokana na sera mpya za usafiri. Fainali za kombe la Dunia 2026 ni mwakani mwezi June. Kadri zinavyokaribia, suala la usafiri wa kimataifa kuelekea Marekani limeanza kujitokeza kama changamoto kwa baadhi ya mataifa. Mashindano hayo yataandaliwa kwa pamoja na Marekani, Kanada na Mexico, huku fainali nyingi zikitarajiwa kufanyika Marekani. Mabadiliko...

Rais Ruto aipongeza Marekani kwa mpango wa kuongeza muda wa AGOA

Rais wa Kenya, William Ruto, ameipongeza serikali ya Marekani kwa mpango wa kuongeza muda wa Mpango wa AGOA. Amesema hatua hiyo italinda mafanikio ya kibiashara ambayo tayari yamepatikana. Mpango huo wa AGOA ulianzishwa mwaka 2000. Unaziwezesha nchi kadhaa za Afrika kupata soko la Marekani bila ushuru kwa bidhaa zilizochaguliwa. AGOA imekuwa nguzo muhimu kwa sekta kama nguo, kilimo na viwanda...

Apple na Google Washutumiwa kwa Kuzuia Uvumbuzi Katika Vivinjari vya Rununu (Mobile Browsers) – Ripoti ya CMA

Biashara | UchumiApple na Google Washutumiwa kwa Kuzuia Uvumbuzi Katika Vivinjari vya Rununu (Mobile Browsers) – Ripoti ya CMA

London, Uingereza – Mei 2025:
Mamlaka ya Ushindani na Masoko ya Uingereza (CMA) imetoa ripoti yenye athari kubwa kwa sekta ya teknolojia, ikihitimisha kuwa makampuni mawili makubwa — Apple na Google — yamekuwa kikwazo kwa uvumbuzi na ushindani katika soko la vivinjari vya rununu (mobile browsers).

Katika ripoti hiyo ya mwisho iliyotolewa Jumatano, CMA inalaumu sera za Apple zinazowalazimisha watengenezaji wa vivinjari vya iOS kutumia injini ya kivinjari cha WebKit, hali inayopendelea kivinjari cha Safari na kudhoofisha uwezo wa ushindani wa vivinjari vingine. Vilevile, imeangazia mapungufu katika uwezo wa programu nyingine kuvinjari kwa uhuru pamoja na Safari kuwekwa kama chaguo-msingi kwenye iPhones.

Kwa upande wa Google, uchunguzi umebaini kuwa kivinjari cha Chrome kimewekwa kama default kwenye vifaa vingi vya Android. Zaidi ya hapo, Google inalipa kiasi kikubwa cha mapato ya utafutaji kwa Apple ili kuendelea kuwa injini ya utafutaji chaguo-msingi kwenye iPhones, jambo ambalo linapunguza motisha ya mashindano baina yao.

“Ushindani kati ya vivinjari vya rununu haufanyi kazi kama inavyotakiwa, na hali hii inakwamisha uvumbuzi nchini Uingereza,” alisema Margot Daly, mwenyekiti wa kikundi maalum cha CMA.

Athari kwa Watumiaji na Sekta ya Kidijitali

Ripoti inasisitiza kuwa kwa pamoja, Apple na Google wanatawala soko la vivinjari kwa kiasi kikubwa — Safari pekee inakadiriwa kushikilia asilimia 88 ya matumizi ya vivinjari kwenye vifaa vya Apple. Hali hii inafanya kuwa vigumu kwa watoa huduma wapya kuvutia watumiaji au kuleta teknolojia mbadala.

Majibu ya Apple na Google

Apple imejibu kwa tahadhari, ikisema:

“Tunaamini katika mazingira ya ushindani na uvumbuzi. Tuna wasiwasi kuwa mapendekezo haya yanaweza kuhatarisha faragha, usalama, na matumizi bora kwa wateja wetu.”

Kwa sasa, CMA haijachukua hatua za moja kwa moja. Badala yake, imezindua uchunguzi tofauti kwa kampuni zote mbili ili kubaini iwapo zinatawala soko la kidijitali kwa namna ya “kifedha na kimkakati.” Ikiwa zitapatikana na hatia, Apple na Google zinaweza kuwekewa masharti magumu ya kisheria au kutozwa faini inayoweza kufikia hadi asilimia 10 ya mapato ya kila mwaka.

Uchunguzi huo unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Check out our other content

Check out other tags:

Most Popular Articles