Thursday, January 15, 2026
26.1 C
Dar es Salaam

Baadhi ya Nchi Kushindwa Kupeleka Mashabiki Kombe la Dunia 2026

Huu ni muhtasari wa nchi zinazoweza kushindwa kupeleka mashabiki nchini Marekani kutokana na sera mpya za usafiri. Fainali za kombe la Dunia 2026 ni mwakani mwezi June. Kadri zinavyokaribia, suala la usafiri wa kimataifa kuelekea Marekani limeanza kujitokeza kama changamoto kwa baadhi ya mataifa. Mashindano hayo yataandaliwa kwa pamoja na Marekani, Kanada na Mexico, huku fainali nyingi zikitarajiwa kufanyika Marekani. Mabadiliko...

Rais Ruto aipongeza Marekani kwa mpango wa kuongeza muda wa AGOA

Rais wa Kenya, William Ruto, ameipongeza serikali ya Marekani kwa mpango wa kuongeza muda wa Mpango wa AGOA. Amesema hatua hiyo italinda mafanikio ya kibiashara ambayo tayari yamepatikana. Mpango huo wa AGOA ulianzishwa mwaka 2000. Unaziwezesha nchi kadhaa za Afrika kupata soko la Marekani bila ushuru kwa bidhaa zilizochaguliwa. AGOA imekuwa nguzo muhimu kwa sekta kama nguo, kilimo na viwanda...

Tume ya Uchaguzi Guinea Bissau CNE Yatangaza Matokeo ya Uchaguzi Kuharibika

Muhtasari wa Matukio Tume ya uchaguzi ya Guinea-Bissau imesema haiwezi kutangaza matokeo ya uchaguzi wa 23 Novemba 2025. Ballots, fomu za hesabu na vifaa vya kompyuta vilikamatwa. Server iliyohifadhi matokeo pia iliharibiwa. Makao ya CNE yalishambuliwa siku moja kabla ya kutangaza matokeo ya muda. Baada ya tukio hilo, jeshi lilitangaza kujidhibiti serikalini. Jeshi lilimtangaza Horta Nta Na Man kama rais wa mpito...

Watu 11 wafariki, 14 wajeruhiwa katika tukio la mauaji Pretoria, Afrika Kusini

Habari FastaWatu 11 wafariki, 14 wajeruhiwa katika tukio la mauaji Pretoria, Afrika Kusini

Takribani watu 11 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa baada ya tukio la ufyatuaji risasi lililotokea mapema Jumamosi asubuhi Afrika Kusini. Tukio hilo limesababisha mauaji jijini Pretoria.

Kwa mujibu wa polisi, tukio hilo lilitokea majira ya saa 4:00 asubuhi katika hosteli ya Saulsville, iliyopo Atteridgeville, magharibi mwa Pretoria.

Miongoni mwa waliopoteza maisha ni watoto watatu. Polisi wamedhibitisha kuwa mvulana wa miaka mitatu alifariki, pamoja na mvulana wa miaka 12 na msichana wa miaka 16.

Walioumia walikimbizwa hospitalini kwa ajili ya matibabu. Hadi sasa, hakuna taarifa kamili kuhusu hali zao au iwapo kuna waliokamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Maafisa wa usalama wamesema uchunguzi unaendelea kubaini chanzo cha tukio na wahusika waliotekeleza shambulizi hilo.

Afrika Kusini ina historia ya muda mrefu ya matukio ya uhalifu unaohusiana na silaha za moto. Nchi hiyo pia ina mojawapo ya viwango vya juu zaidi vya mauaji duniani, kwa mujibu wa takwimu za usalama.

Tukio hili limeongeza wasiwasi kuhusu usalama wa raia, hasa katika maeneo ya makazi yenye watu wengi. Mauaji na uhalifu si jambo geni Pretoria na Afrika Kusini kiujumla.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Check out our other content

Check out other tags:

Most Popular Articles